Wednesday, July 3, 2013

MACHANGUDOA WAULAANI UJIO WA OBAMA....WANADAI HAUKUWA NA PESA IKILINGANISHWA NA ULE WA BUSH


Katika hali ilisiyokuwa ya kawaida,  machangudoa wameulalamikia ujio wa Rais Barack Obama kwa kile kinachodaiwa  kuwa  haukuwa na faida yoyote kwa kukosa dili za pesa.



" Tumesikitishwa sana na ujio wa Obama kwani tulikuwa tumejipanga kupiga hela ndefu sana .
"Bahati mbaya watu  wake tuliokuwa tunategemea kuwanasa walikuwa busy na wale  wa  mikoani  walizuiwa" Walisema akina dada hao.
 
Machungudoa hao wanadai  kuwa  kipindi cha Bush alipokuwa Rais ambaye alikaa nchini karibu wiki moja walinufaika sana ambapo wengi wao walijenga majumba kwa pesa za ziara ya Bush .

No comments:

Post a Comment