Wednesday, July 3, 2013

"SUGU AMESAFISHWA KWA KUMTUKANA WAZIRI MKUU. FIKIRIA TUSI HILO LINGETOKA KWA MLALA HOI "...MBWANA


KILA mtu anajua kuwa sheria na haki ni vitu viwili tofauti. Usilazimishe kupata haki, kwasababu sheria imeonyesha juu ya madai yako. Kufanya hivyo ni kujipotezea muda wako unaoweza kuutumia katika kazi nyingine za maendeleo yako.

Pamoja na  yote hayo, lakini wakati mwingine si sahihi kujificha kwenye mhimili wa kisheria kwa kufanya mambo ambayo ni tofauti katika jamii. Kila mmoja anapaswa kuishi kwa upendo bila kuweka u-mimi, vyama vyetu na mengineyo pia.


Nasema haya baada ya Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu kama ‘Sugu’kutoka (CHADEMA)kuachiwa huru na Mahakama ya Wilaya ya Mkoa wa Dodoma, kwa madai kuwa hati ya mashitaka ina mapungufu kisheria.


Sugu alipandishwa kizimbani katika mahakama hiyo, mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mkoa wa Dodoma, Elinaza Luvanda na kusomewa shitaka linalomkabili kuhusu kutoa lugha ya matusi katika mtandao wa kijamii, moja ya vitu vinavyotumiwa vibaya na watu wengi.

Katika mitandao hiyo, kila mmoja anaandika kile anachojisikia, bila kujali faida au hasara inayopatikana kwa kuandika upupu wake.


Sugu aliandika hivi;”Tanzania haijawahi kupata Waziri Mkuu mpumbavu kama Pinda”.

MACHANGUDOA WAULAANI UJIO WA OBAMA....WANADAI HAUKUWA NA PESA IKILINGANISHWA NA ULE WA BUSH


Katika hali ilisiyokuwa ya kawaida,  machangudoa wameulalamikia ujio wa Rais Barack Obama kwa kile kinachodaiwa  kuwa  haukuwa na faida yoyote kwa kukosa dili za pesa.



" Tumesikitishwa sana na ujio wa Obama kwani tulikuwa tumejipanga kupiga hela ndefu sana .
"Bahati mbaya watu  wake tuliokuwa tunategemea kuwanasa walikuwa busy na wale  wa  mikoani  walizuiwa" Walisema akina dada hao.
 
Machungudoa hao wanadai  kuwa  kipindi cha Bush alipokuwa Rais ambaye alikaa nchini karibu wiki moja walinufaika sana ambapo wengi wao walijenga majumba kwa pesa za ziara ya Bush .

Monday, May 20, 2013

WALIOBOMOLEWA NYUMBA ZAO KIJIJI CHA KIVULE KUMVAMIA WAZIRI MKUU

Ni sehemu ya Nyumba kubwa iliyokuwepo katika Maeneo ya  Kitongoji cha Mkombozi kijiji cha Kivule jijini Dar es Salaam, iliyobomolewa  na Polisi kwa Madai kuwa wananchi hao hawaruhusiwi kukaa katika Maeneo hayo, ambapo Nyumba zaidi ya 300 zilibomolewa na wahanga hao wamepanga kwenda kwa Waziri Mkuu kupata haki yao baada ya kuomba msaada katika ngazi zote za Chini na kutopata Msaada wowote.

Takriban Wakazi zaidi ya 500 katika kijiji cha Mkombozi kata ya Kivule Jimbo la Ukonga jijini Dar es Salaam wasiokuwa na makazi ya kuishi baada ya Kubomolewa nyumba zao na  Polisi kwa madai ya kuwa hawastahili kuishi maeneo hayo wanajiandaa kufanya Maandamano ya kwenda katika Ofisi ya waziri Mkuu kupeleka malalamiko yao kwa ajili ya kupata haki yao.
Akizungumza katika kikao cha wakazi hao Katibu  wa wahanga hao, Mwanaharakati  Julius  Zephania, alisema kuwa,  wanaamini kuwa haki yao ipo ila ni swala la wao kuipigania.
Zefania alisema kuwa, siku ya kwenda kwa Waziri mkuu imekaribia ambayo wanaamini kuwa, ndio mkombozi wao ambapo alimwomba waziri mkuu watakapofika wawaikiliza na kuwahurumia kwani nao ni wananchi kama walivyo watu wengine.
Naye Mwenyikiti wa wahanga hao, Bw, Habibu Iddi amesema kuwa, sababu zilizofanywa wao kubomolewa nyumba zao ni kwamba hawaruhusiwi kukaa katika Eneo hilo na kwamba  anayewanyanyasa ni mtu mmoja walio mtaja kwa Majina ya Jordan Rugimbana ambaye ni mkuu wa wilaya ya Kinondoni ambaye anadai kuwa Eneo hilo ni lake.
“Tunamshangaa sana huyu mtu kutubomolea nyumba zetu , sasa sisi umefika wakati wetu wa kupata haki yetu na ni lazima tufike kwa  Waziri Mkuu kwani tunaamini ndiye pekee anayeweza kutusikiliza.
MAASINDA ilimtafuta Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Bw,  Joseph Gasaya ambapo amesema kuwa, swala hilo ameshalifikisha katika ngazi za juu lakini bado anazungushwazungushwa ambapo alisema kuwa ni haki ya wananchi wake kwenda Mahakamani.

Mwanaharakati  Julius  Zephania,ambaye ni katibu wa wahanga waliobomolewa nyumba zao akiwashauri Wananchi wake kufanya maandamano Makubwa na ya amani kwenda kwa Waziri Mkuu kudai haki yao.

Utafikiri hapakuwa na jengo

BIASHARA YA UKAHABA YASHAMIRI DODOMA,MAKAHABA WA DAR NAO WAPIGA KAMBI HUKO KATIKA KIPINDI HIKI CHA BUNGE...!!

BIASHARA ya ngono katika mji wa Dodoma imeshika kasi kubwa ambapo imebainika kuwa wateja wakubwa ni watumishi wa serikali, wanasiasa na madereva.
Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima umebaini kuwa katika biashara hiyo kuna makundi mbalimbali yanayotofautiana kwa malipo ya biashara hiyo.

Wapo wanafunzi wa vyuo vikuu na wanawake ambao wamedai kuwa wanalazimika kufanya biashara hiyo kutokana na kubanwa na maisha, hususani katika marejesho ya mikopo wanaichukua kutoka katika taasisi mbalimbali ya kifedha.

Mmoja wa wafanyabiashara ya ngono (jina tunalo) bila kujua anaongea na nani, alieleza kuwa kwa sasa katika mji wa Dodoma kuna ushindani mkubwa wa biashara ya ngono kwani wanafunzi wa vyuo vikuu vya mjini hapa vimeteka soko hilo.

Alisema kutokana na ushindani huo kwa sasa kima cha chini ni sh 7,000 kwa mchepuo mmoja na sh 30,000 hadi 40,000 kwa kulala.

Mfanyabiashara huyo alieleza kuwa wateja wakubwa wa ngono ni wafanyakazi wa serikali, wanasiasa (wabunge), madereva pamoja na wafanyakazi wa benki.



Bila hofu mfanyabiashara huyo alieleza kuwa kuanzia muda wa saa tatu hadi sita usiku wanajipanga katika maeneo ya biashara na yanapofika magari hujipanga mbele ya gari ili mteja amchague anayemtaka.

“Hapa tupo wengi, lakini pia wengine ni wafanyakazi wa serikali wanakuja hapa kujiuza, wanafunzi wa vyuo vikuu nao hivyo hivyo… Mimi nipo hapa ninakuja kwa siku maalum ambazo ninakuwa nimekwama.

“Ninakabiliwa na masuala ya mikopo. Unajua hapa tupo kama kumi akina mama ambao tumekopa mikopo katika taasisi mbalimbali, lakini mitaji inapoyumba unajiuliza utapata wapi, unalazimika kuja kufanya biashara,” alisema.

Aliongeza kuwa kwa kawaida mtu mmoja anaweza kufanya ngono na watu wasiopungua saba kwa siku, hivyo ana uhakika wa kujipatia kiasi cha sh 70,000 iwapo siku itakuwa nzuri.

Alibainisha kuwa na kama siku ni mbaya anaweza kupata kiasi cha sh 49,000 iwapo atalipwa sh 7,000 kwa mchepuo mmoja.Uchunguzi wa kina uliofanyika umebaini maeneo ambayo yana wasichana wengi ambao ni makahaba ni Chako Nichako, Double H na Mtaa wa Uhindini ambako kuna gesti maarufu kwa kufanya biashara hiyo.

Hata hivyo, imebainika kuwa makahaba wa vyuo vikuu viwango vyao ni kuanzia sh 200,000 kulala na sh 30,000 kwa mchepuo mmoja.

Mmoja wa waendesha bodaboda ambaye hakutaka jina lake litajwe, alieleza kuwa katika biashara hiyo yapo maeneo ambayo kwa sasa kuna wakala wenye kundi kubwa la wasichana anaowauza.

Wakati biashara ya ngono ikionekana kushamiri, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rehema Nchimbi alishatangaza kuwawinda na kuwatia kwenye mikono ya sheria wale wanaojihusisha nayo.

Hata hivyo, kauli hiyo inaonekana kukosa mashiko kwani biashara hiyo inazidi kushamiri siku hadi siku.

Imeandikwa na

Danson Kaijage, Dodoma

HIVI NDIVYO WANAJANGWANI WALIVYOMLAKI KIPENZI CHAO MRISHO NGASSA..!

Ngassa amezungumza kwa mara ya kwanza na kuthibitisha kwamba kweli amesaini Yanga.
“Ni kweli nimesaini Yanga, nisingeweza kuzungumzia suala hilo wakati nina mkataba ambao ulikuwa haujamalizika.
“Lakini baada ya mechi ya mwisho ya ligi, sasa niko huru kuanza kuutumikia mkataba wangu mpya,” alisema.
Mashabiki wa Yanga walimchukua Ngassa na kumvisha jezi ya njano na kijani, mara tu baada ya kumalizika kwa mechi kati ya Yanga na Simba kwenye Uwanja wa Taifa, jana.
Mashabiki hao walimvisha jezi hiyo na kumbeba na kumbeba na kuondoka naye hadi nje ya uwanja.
Azam FC ilimpeleka Simba kwa mkopo, lakini Simba imekuwa ikisema ilimuongezea mkataba wa mwaka mmoja na kumlipa Sh milioni 30 pamoja na gari.


Kama unahitaji picha ambazo alikuwa akisani mkataba huo mpya wa Yanga ingia hapa www.facebook.com/edwintanzania

Saturday, May 18, 2013

HOFU YATANDA BUNGENI KUTOKANA NA TETESI ZA SHAMBULIO LA KIGAIDI MJINI DODOMA




Hali ya wasiwasi imelikumba Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya kuwepo kwa tetesi ya shambulio la kigaidi katika maeneo ya Bunge.

Hali hiyo inafuatia ujumbe mfupi wa maneno uliosambazwa, ukitaadharisha kuwa kuna tukio la kigaidi limepangwa kufanywa katika eneo la Bunge.

Ujumbe huo uliosambazwa kwenye simu za baadhi ya wabunge ulisomeka hivi:-

"Kuna kikundi kina mkakati wa kufanya shambulio la bomu bungeni Dodoma na msikiti wa Msavu Morogoro. Ni ndani ya muda mfupi wakati bado vikao vya Bunge,"ailisema sehemu ya ujumbe huo.


Habari zaidi zinasema kuwa tayari jeshi la polisi imefanikiwa kupata mtu aliyetuma ujumbe huo, ambaye anadaiwa kutuma kutoka mikoa ya kanda ya kaskazini na wamefanikiwa kumleta mjini hapa kwa mahojiano zaidi ili kufanikisha upelelezi.



Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge, Mussa Azzan Zungu, juzi alilitangazia Bunge hali hiyo ya hatari  wakati wabunge wakiendelea na mjadala wa hotuba ya makadirio ya matumizi wizara ya Uchukuzi ya mwaka 2013/14, na kulazimika kurudia tangazo hilo wakati akiharisha Bunge.  


“Waheshimiwa wabunge wote mnaombwa kuanzia kesho tarehe 17, mwezi huu, mwaka huu, kutoegesha magari yenu pembezoni mwa uzio unaozunguka ofisi ya bunge hapa Dodoma…Badala yake magari hayo yaingizwe katika geti la eneo la maegesho ya waheshimiwa wabunge ndani ya viwanja vya Bunge” alisema Zungu

Alisema mbunge yeyote atakaye taka kuegesha gari lake nje ya ofisi, anaombwa aegeshe ng’ambo ya upande wa kaskazini wa barabara itokayo jijini Dar es Salaam.


Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi alisema ulinzi umeimarishwa katika eneo lote la Bunge kuhakikisha hakuna chochote cha hatari kinachoweza kutokea.

“Vijana wangu wanafanya kazi yao vyema na iwapo kuna tishio lolote lile litafanyiwa kazi,” alisema Dk Nchimbi

Dk Nchimbi alisema ulinzi utaendelea kuimarishwa katika eneo hilo kuliko wakati wowote ambao Bunge limewahi kuwekwa katika usalama.

WAKAZI ZAIDI YA 500 HAWANA PA KUISHI BAADA YA KUBOMOLEWA NYUMBA ZAO

Mwanamama aliyenaswa na Kamera yetu Maeneo ya Kivule jijini Dar es Salaam akiwa analia baada ya Polisi kubomoa makazi yake katika Maeneo hayo jambo lililopelekea Mpaka sasahivi Mwanadada huyu kukosa pa kuishi.
 Katika Kuitunza Amani ya Tanzania  inayoaminika kuwa imejaa Tele, Bado kuna wananchi wengine ambao ni Watanzania Wenzitu hawaifaidi na wanaona kama Amani haipo Kabisa kutoka na na Hali wanayoishi nao.

Hayo yametokea hivi karibuni, katika Kata ya Kivule jijini Dar es Salaam Baada ya Polisi kuvunja nyumba za Wakazi zaidi ya Miatano na kuharibu mali zao, ambapo, mpaka hivi sasa Wakazi hao hawana Pakuishi.

Chanzo cha Polisi kuwabomolea Makazi yao ni Mgogoro uliopo katika Eneo hilo ambao tayari kesi ipo mahakamani lakini polisi wameingilia uhuru wa Mahakama na kuvunja kesi ikiwa bado ipo Mahakamani.

Maasinda imeshuhudia baadhi ya picha za Eneo hilo, na kuona watu wakiishi kwa tabu kutokana na kukosa Makazi baada ya kubomolewa.
Hii ni Moja ya Nyumba iliyojengwa kwa Muda ili kuwasitiri wananchi waliobomolewa nyumba zao, mahali ilipo nyumba hiyo ya Muda kulikuwa na nyumba kubwa na nzuri iliyobomolewa na Askari hao.

Jionee Mwenyewe

Watu wazima waliotafuta hela kwa jasho jingi wakafanikiwa wakimwaga Machozi hadharani baada ya kubomolewa nyumba zao.

Yalitumika Mabomu kubomolewa Nyumba hizo hili ni Moja ya Kasha la Bomu

MAASINDA inatarajia kufika eneola Tukio na itawaletea hali ilivyo katika Maeneo hayo