Monday, September 24, 2012

MALECELA ATAKA WENYE FEDHA WAHOJIWE








WAZIRI mkuu mstaafu John Samwel Malecela, ametaka kuchukuliwa kwa hatuia za kuwafikisha mahakamani watu wotewenye fedha ambao hazijulikani  namna walivyopata.
Akizungumza katika kipindi cha dakika 45 leo kinachorushwa kila siku ya jumatatu na kituo cha Luninga cha ITV malelecela amesema watu hao wanapaswa kuhojiwa kwa ajili ya kujua vyanzo vyao kama havihusiani na ufisadi unaoendelea nchini.
Amesema alipokuwa nje ya nchi alishangaa kuambiwa na wenyeji wake kuwa kuna mtanzania aliyefika huko na kununua gari aina ya Range Rover  kisha akapakia katika ndege kitu alichoeleza si cha kawaida hata katika nchi zilizoendelea
Akizungumzia elimu Malecela amesema hatua ya kuwepo kwa shule za sekondari katika kila kata linafaa kupongezwa na kinachopaswa ni kuiboresha zaidi kwa ajili ya kuwasaidia vijana
Alitolea mifano ya baadhi ya shule za kata zilizoweza kuingia katika shule 20 bora za kitaifa na kueleza hilo si jambo la kupuuzwa.
Kuhusu umeme alisema serikali ya awamu ya kwanza iliamini katika umeme wa vyanzo vya maji na sasa viongozi waliopo wana wajibu wa kutafuta umeme mbadala itakayowezesha nchi kufanya kazi kwa muda wote
Amesema kama watanzania wataamua kujitoa kwa kununua umeme jua leo hii kusingekuwa na kelele za kupigania umeme wa tanesco

No comments:

Post a Comment