Wednesday, November 14, 2012

STAR TIMES WASHUSHA GHARAMA ZA BIDHAA ZAKE

Kufuatia maelekezo ya TCRA mfumo wa analogia utakoma kabisa kutumika hapa nchini Tanzania tarehe 31 Desemba, 2012. Baada ya tarehe hiyo mfumo rasmi wa utangazaji wa matangazo ya televisheni utakuwa katika mfumo wa digitali. Kwa hali hiyo watanzania wanaotumia mfumo wa analogia kwa sasa wanalazimika kujiandaa mapema na mabadiliko hayo kwa kununua ving’amuzi au televisheni za digitali katika maduka ya starTimes au kwa mawakala wetu popote walipo nchini.
Ili kuweza kuingia mapema katika mfumo mpya wa utangazaji wa television wa digitali, Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) lilingia ubia na kampuni kutoka China ijulikanayo kama STAR COMMUNICATION NETWORK COMPANY LTD na kufungua kampuni hapa nchini kwa pamoja iitwayo STAR MEDIA (TANZANIA) LTD kwa jina la kibiashara StarTimes.
Wajibuwa kampuni ya StarTimes ni kuanzisha mfumo mpya wa kurusha matangazo ya hewani kwa mfumo wa   digitali nchini Tanzania. Startimes kwa sasa inapenda kuwatangazia wananchi upunguzaji wa bei zake kwa mfano; King’amuzi kimepungua bei kwa asilimia zaidi ya 30 kutoka 70,000/= mpakakufikia 39,000/= katika kusheherekea sikukuu hii ya Christmas kuanzia 15 November 2012 mpaka 31 January 2013. King’amuzi hicho kitakuwa na (warranty) udhamini wa mwaka mmoja na kitapatikana maduka yetu yote ya startimes Tanzania ukijumuisha namawakala wetu popote walipo.
Wateja pia wanaweza kuchagua kifurushi wakipendacho, kwa kuwa kampuni hivi karibuni iliongeza chaneli za ndani na za kimataifa katika orodha yake yavifurushi nakufikisha idadi ya zaidi chaneli 54. Viwango vya malipo vimepangwa katika makundi yafuatayo:
  • Kifurushi cha MAMBO kwa TSh. 9,000/=, chaneli 30+
  • Kifurushi cha UHURU kwa TSh. 18,000/=, chaneli 45+
  • Kifurushi cha KILI kwa TSh. 36,000/=, chaneli 54+
Kwa sasa kampuni ya StarTimes inaendelea na ujenzi wa vituo vipya vya kurusha matangazo ya digitali katika mji ya Morogoro na visiwani Zanzibar na baadae mwaka ujao itaendelea kufunga mitambo hiyo katika mikoa mingine.  Kwa vituo vilivyokwisha jengwa mpaka sasa ni katika miji ya Dar-es-salaam, Dodoma, Mwanza, Mbeya, Arusha, Moshi naTanga.
Katika jitihada za kuwaburudisha Watanzania kufurahia michezo kutoka dunia kote, StarTimes sasa inarusha mechi nyingi na nzuri za Barani Ulaya kupitia chaneli ya DTV. Hata hivyo Startimes itazindua ofa maalum ya Christmas itakayoanza tarehe 15 Novemba, 2012 hadi 31 Januari, 2013 kama ifuatavyo:
  1. Wateja wa zamani: Ukiongeza salio kwa miezi mitatu unazawadiwa mwezi mmoja bure.
  2. Kingamuzi:  Ukinunua king’amuzi kimoja kwa TSh. 39,000/=, una uamuzi wa kuchagua kifurushi unachokitaka kati ya MAMBO, UHURU.
  3. TV ya digitali 21”CRT:  Kutoka TSh. 285,000/= hadi TSh. 239,000/=, unapata pamoja na mwezi mmoja kifurushi cha Uhuru.
  4. TV ya digitali  24” LCD: Kutoka Tsh. 544,000/= hadi TSh. 449,000/=, unapata pamoja na mwezi mmoja wa kifushi cha Uhuru.
  5. TV ya digitali 32”LCD: kutoka shilingi 835,000/= hadi TSh. 699,000/=, unapata pamoja na mwezi mmoja kifurushi cha KILI.
  6. TV ya  42” LED: Unapata pamoja na king’amuzi kimoja bure kwa TSh. 1,300,000/=, ikijumishwa na mwezi mmoja wa kifurushi cha KILI.
Zawad izaidi zitatolewa kwa wateja wapya na wale wazamani.
Katika kusherekea sikukuu ya Christmas StarTimes inawapa nafasi kubwa Watanzania wote kusherekea sikukuu hii pamoja na familia zenu namarafiki hasa katika kipindi hiki cha sikuu.
Kadri tarehe ya kufunga mfumo wa analog inavyokaribia StarTimes imejitahidi kupunguza gharama zake za huduma na bidhaa zake tofauti na makampuni mengine.
Mpaka sasa StarTimes ina wateja wapatao million 7 duniani kote ambapo kwa Afrika inawateja wapatao milioni 1.5 kwa nchikumi za kiafrika.Tanzania ni nchi mojawapo inayopata huduma hii ya mfumo wa digitali kwa bei nafuu na wananchi kufurahia thamani ya malipo yao.
Kwa taarifa zaidi tembelea madukaya StarTimes pamoja na mawakala wetu wa StarTimes popote walipo.

No comments:

Post a Comment