Saturday, January 12, 2013

MEYA WA KINONDONI AZINDUA UJENZI WA DARAJA MBEZI JUU MTAA WA NDUMBWI

Ujenzi wa Daraja la Mbezi Ndumbwi ukiendele hawa ni baadhi ya waandishi wa habari pamoja na mashuhuda waliomsindikiza Meya wa Kinondoni katika Uzinduzi wa Daraja hilo

Meya wa Manispaa ya Kinondono Mstahiki Yusuph Mwenda(katikati aliyevaa shati la Drafti)  akiingia katikati ya Daraja la Mbezi Ndumbwi lililozinduliwa leo jijini Dar es Salaam akiwa anasindikizwa na viongozi wa Kata na Mtaa huo kushoto kwake ni  Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa ya Mbezi Ndumbwi Bw, Salustian Kimario na aliye mbele ni Diwani wa Kata ya Mbezi  Juu.

Meya wa Manispaa ya Kinondono Mstahiki Yusuph Mwenda wakishangaa ujenzi unaoendelea akiwa na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa ya Mbezi Ndumbwi Bw, Salustian Kimario

Mkandarasi wa Manispaa ya Kinondoni Bw Gerald Urio akimuelekeza Meya namna Makandarasi watakavyofanya kazi kuhaklikisha kuwa Daraja hilo linakamilika ndani ya Siku 90 kuanzia leo.

Baadaye Meya aliwahutubia wakazi wa Mbezi Ndumbwi

No comments:

Post a Comment